emblem

The United Republic of Tanzania

The National Museum of Tanzania (NMT)

BG IMAGE

Welcome to National Museum

Dr. Rashid Mfaume Kawawa Museum Exhibition

Dr. Rashid Mfaume Kawawa Museum Exhibition

Makumbusho ya Kumbukumbu ya Dkt. Rashid Mfaume Kawawa ni Tawi la Makumbusho ya Taifa la Tanzania. Makumbusho haya yalifunguliwa rasmi 27 /02/2017. Makumbusho ya Dkt. Rashid Mfaume Kawawa inapatikana Mtaa wa Kawawa, eneo la Bombambili, Wilaya ya Songea, Mkoa wa Ruvuma. Makumbusho haya yanahifadhi historia kuhusu maisha binafsi, maisha ya kisiasa na vitu mbali mbali alivyotumia aliyekuwa Kiongozi mwenye utumishi adhimu na uliotukuka Dkt. Rashid Mfaume Kawawa “Simba wa Vita” wakati akiwa Waziri Mkuu wa Pili na Makamu wa Rais na Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (awali Tanganyika). Maisha yake yanaonekana katika vitu alivyotumia enzi za uhai wake.


Sehemu ya Maonesho yaliyomo ndani ya Makumbusho ya Dkt. Rashid Mfaume Kawawa Mjini Songea Mkoani Ruvuma.



Kiti kilichotengenezwa na mti wa mnazi, kilitumiwa na Dkt. Rashid Mfaume Kawawa na sasa ni sehemu ya onesho katika Makumbusho, Mjini Songea, Mkoani Ruvuma.



Mtambo wa kuoneshea Sinema ukiwa na mkanda wa Filamu ya Muhogo Mchungu iliyokuwa Filamu ya kwanza ya kiafrika nchini Tanganyika (Tanzania), ni sehemu yavioneshwa vilivyopo katika Makumbusho ya Dkt. Rashid Mfaume Kawawa iliyopo Mjini Songea, Mkoani Ruvuma.